back

YALIYOMA

next page

 

Utangulizi

Kuambatana na Hekima ya Mwenyezi Mungu

Baada ya hayo, jua ya kwamba hekima ya Mwen-yezi Mungu inamlazimu yeye kuwaongoza watu katika kuyafikia yaliyo mema na yenye maslahi kwao, humu duniani na huko akhera, ili waweze kuupata ukamilifu unaoambatana na lengo la maumbile yao, ambao ni, kumjua Mwenyezi Mungu na kuupata ukurubifu wake.

Uongofu wake unapatikana kwa njia ya wahyi na kuviteremsha vitabu vitukufu na kwa kuwatuma manabii na marasuli na kuwateua mawasii. Huu uon-gofu umeendelea kupatikana tangu alipoumbwa Nabii Adam (a.s) na wala watu hawakuwahi kutouhitajia kamwe katika zama mojawapo, kwani akili zao hazikuyajua maslahi yao yote (yanayowafaa) ya humu duniani na huko akhera, bali daima walikuwa ni wenye kuuhitajia msaada wa Mwenyezi Mungu kwa kupitia wahyi na mitume watukufu. Nao wahyi hautengamani na Mtume bali vyote viwili ni kama mapacha, vina-shirikiana katika kuwafikishia watu uongofu wao.

Basi kila Mtume alikuwa na wahyi na kila wahyi ulikuwa na Mtume. Naam, kuteuliwe kwa mitume (manabii) na wajumbe (marasuli) kulipo khitimishwa, Kitabu kitukufu kilichokuwa kimeteremshwa na Mwenyezi Mungu kilibaki mikononi mwa wasii, kwa-ni watu walikuwa ni wenye kukihitajia daima Kitabu hiki pamoja na mfafanuzi wa yaliyomo ndani yake, ambaye ni mwalimu na mlezi na mtakasaji.

Hili ni jambo lenye uhakika linaloungwa mkono na kila mwenye akili safi, pamoja na riwaya (hadithi) zilizo mutawatir (nyingi).

Mwenyezi Mungu (s.w.) kwa kuonyesha mshangao kutokana na kukanusha kwa makafiri amesema;

]وكيف تكفرون وانتم تتلى عليكم آيات الله وفيكم رسوله ومن يعتصم بالله فقد هدى الى صراط مستقيم[

“Na mnakanushaje, hali nyinyi mnasomewa aya za Mwenyezi Mungu na Mtume wake yuko pamoja nanyi? Na mwenye kushikamana Mwenyezi Mungu (sawa sawa) basi yeye amekwisha ongozwa katika njia iliyo-nyooka”.([1])

Yaani, mnakufuruje na kukanusha ilhali aya za Mwenyezi Mungu zasomwa mbele yenu na mjumbe (Rasuli) wake, naye yu pamojo nanyi anawapa mawa-idha na kuwakataza mabaya. Na Mwenye  kushika-mana na Mwenyezi Mungu kwa hakika atakuwa amepata uongofu bila shaka. Kwa hivyo tunaona wazi kuwa aya tukufu inatuthibitishia kuwa kufuru na upotofu havipatikani vinapokuwepo vitu viwili, navyo ni:

kwanza: Aya zinazosomwa, nazo ni Qurani tukufu.

Pili : kuwepo kwa Mtume (s.a.w.a).

Mwenye kuvikhalifu hivi viwili basi amekwisha-potea na kutoka kwenye njia iliyonyooka, kinyume cha mwenye kushikamana na Mwenyezi Mungu kwa kuzipokea aya na kumfuata Mtume (s.a.w.a). Basi huyo amekwishaongoka na kuipata njia iliyonyooka.

Kufuatana na msingi huu wa haki Mtume (s.a.w.a) alitaka kuubainishia umma wa kiislamu njia ya sawa ili wasipotee baada ya kufa kwake, bali waifwate njia iliyonyooka. Na hii ndio sababu hasa ya kuwaongoza katika kukifuata Kitabu cha Mwenyezi Mungu na katika kuwafuata Ahlulbait (a.s), ili kwamba sababu za uongofu na saada yao ya dunia na akhera zidumu kuendelea. Mtume (s.a.w.a) aliwabainishia kwa njia tofauti tofauti na katika sehemu na nyakati zilizona-sibiana na maudhui.

Miongoni mwazo ni; hadithuth thaqalain (Hadithi ya vizito viwili) iliyo maarufu na yenye kuafikiana ma-dhehebu ya kishia na kisunni. Mtume (s.a.w.a) kwa maneno yoliyoko kwenye hadithi hii alitaka kuuongoza umma katika mustakbali wao hadi siku ya kiyama.

 

Hadithuth Thaqalain

Hakuna shaka kuwa hii hadithi inayopatikana kwenye vitaba vya madheheba yote inaelezea kwa uwazi kwamba Mtume (s.a.w.a) hakuupuuza umma wa kiislamu na kuuacha hivi hivi bila ya mwongozo, bali aliwaelezea cheo kitukufu cha Quran na kizazi chake kitoharifu, na kuuwajibishia umma kushika-mana navyo. Kisha akawadhaminia washikanao navyo kuwa hawatapote, na kisha akasisitizia kuwa kamwe havitatengana hadi vitakaporudi kwake huko hodhini mwa kauthar. Kwa maneno haya alibainisha wazi kabisa kutotengana na kutofarikiana kwa kizazi kutokana na Quran, na kutotengana kwa Qurani kuto-kana na kizazi chake. Kisha akauainsishia umma wa kiislamu maregeleo yao katika mambo ya kielemu na katika mambo ya kisiasa.

Haya, pamoja na kuwa hadithi haionyeshi kuwa mambo haya yanahusu zama fulani makhsusi, bali inanyesha kuwa ni wajibu unaoendelea juu ya wais-lamu wote katika kila pembezoni mwa ardhi na katika kila wakati na zama.

Kutokana na haya, na yatakayokuja tunatambua ya kwamba uchunguzi na kufikiria kwa makini kuihusu hadithi hii ni kitu chenye faida kubwa kwetu na kwa ndugu zetu waislamu ambako kutaondosha dhana mbaya zinazosababisha kukhitilafiana na kufarikiana.

Uchunguzi wa hadithi hii unagawanyika katika sehemu zifwatazo.

 

 


([1]) Quran – Aali Imran – 101.

 

index